Thursday 27 February 2014

TANGAZO LA KAZI

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI
Kamishna Mkuu wa Uhamiaji anatangaza nafasi za kazi katika Idara ya Uhamiaji. Nafasi hizo ni Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji, Koplo wa Uhamiaji na Konstebo wa Uhamiaji.
A.      MKAGUZI MSAIDIZI WA UHAMIAJI (Nafasi 70)
         
  • SIFA ZINAZOHITAJIKA
  • Awe na Shahada ya Kwanza au Stashahada ya Juu kutoka Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa  na Serikali katika fani zifuatazo:
Sheria, Uchumi, Biashara, Utawala, Uandishi wa Habari, Ualimu, Usafirishaji, Raslimali Watu, Sayansi ya Kompyuta, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Takwimu, Uchapaji, Uhandisi Majengo na Uhandisi Mitambo.
  • Awe na umri usiozidi miaka 35

  • MAJUKUMU NA KAZI ZA KUFANYA
  • Kusimamia doria sehemu za Mipakani, Bandarini, Vituo vya Mabasi, Treni na sehemu zenye vipenyo vya kuingia na kutoka nchini vikiwemo vya majini
  • Kusimamia shughuli za upelelezi, kuandaa Hati ya Mashitaka na kuendesha mashitaka
  • Kutoa na kupokea fomu mbali mbali za maombi ya Hati za Uhamiaji
  •     Kufanya Ukaguzi wa Mwanzo wa Maombi mbalimbali
  • Kuagiza ufunguaji wa Majalada ya watumiaji
  •  Kupokea na kukagua Hati za Safari, Fomu za Kuingia na Kutoka Nchini
  • Kuidhinisha malipo mbalimbali ya huduma za Uhamiaji kwa wanaostahili
  • Kutunza kumbukumbu za ruhusa za watu wanaoingia na kutoka nchini
  • Kukusanya, kusimamia na kutunza takwimu za Uhamiaji na Uraia
  • Kuandaa majibu ya maombi yote ya huduma za uhamiaji yaliyokubaliwa au kukataliwa

B:      KOPLO WA UHAMIAJI (Nafasi 100)      
1.      SIFA ZINAZOHITAJIKA:
  • Awe amehitimu Kidato cha Sita na kufaulu
  • Awe na umri usiozidi miaka 30
C.      KONSTEBO WA UHAMIAJI (Nafasi 100)
1.      SIFA ZINAZOHITAJIKA:
  • Awe amehitimu Kidato cha Nne na kufaulu
  • Awe na umri usiozidi miaka 25
D:      SIFA ZA ZIADA: KOPLO/KONSTEBO WA UHAMIAJI
  • Cheti cha Ufundi Stadi (Full Technical Certificate) kwenye fani ya Umeme na Mitambo
  • Cheti au Stashahada ya Uhaziri (Certificate or Diploma in Secretarial Studies) kutoka Chuo kinachotambulika na Serikali
  • Cheti au Stashahada ya Kutunza Kumbukumbu (Certificate in Records Management) kutoka Chuo kinachotambulika na Serikali
  • Cheti au Stashahada ya Takwimu (Certificate or Diploma in Statatistics ) Kutoka Chuo kinachotambulika na Serikali.
  • Cheti au Stashahada ya Vyombo vya Majini (Certificate or Diploma in Marine Transportation and Operations) kutoka Chuo kinachotambulika na Serikali
  • Cheti au Stashahada katika fani ya Uchapaji (Printing)
  • Ujuzi na Elimu ya Kompyuta na Uandishi mzuri utazingatiwa
  • Cheti cha Ufundi Makanika,Kozi ya juu ya Udereva na Leseni ya Udereva Daraja C

E.       MAJUKUMU NA KAZI ZA KUFANYA
  •  Kufungua, kupanga na kutunza majalada ya huduma mbalimbali za Uhamiaji
  •      Kuandika Hati mbalimbali za Uhamiaji
  • Kufanya doria sehemu za Mipakani, Bandarini, Vituo vya Mabasi, Treni na sehemu zenye vipenyo vya kuingia na kutoka nchini vikiwemo vya majini.
  • Kusindikiza watuhumiwa wa kesi za Uhamiaji Mahakamani pamoja na wageni wanaofukuzwa nchini
  • Kufanya ukaguzi kwenye mahoteli, nyumba za kulala wageni na sehemu za biashara.
  • Kuchapa au kuandika kwa kompyuta barua au nyaraka mbalimbali zinazohusu kazi za kila siku za Uhamiaji.
  • Kufanya matengenezo/ukarabati wa mitambo na vitendea kazi vya Uhamiaji
  • Kuandaa na kutunza takwimu za huduma mbalimbali za uhamiaji
F.       MAOMBI YOTE YAWE NA VIAMBATISHO VIFUATAVYO:
  • Nakala za vyeti vya kuhitimu masomo kwa mujibu wa sifa zilizotajwa
  • Nakala ya Cheti cha Kumaliza Elimu ya Msingi
  • Nakala ya Cheti cha Kuzaliwa
  • Picha mbili (Passport Size)
  • Barua ya Utambulisho kutoka kwa Mwenyekiti wa Serikali za Mitaa
G.      UTARATIBU WA KUTUMA MAOMBI
Maombi yote yapitie posta na barua za maombi ziandikwe kwa mkono.
  • Maombi ya nafasi ya Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji yatumwe kwa:

KATIBU MKUU,
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI,
S.L.P. 9223,
DAR ES SALAAM
  • Maombi ya nafasi ya Koplo wa Uhamiaji na Konstebo wa Uhamiaji yatumwe kwa:

KAMISHNA MKUU WA UHAMIAJI,
S.L.P. 512,
DAR ES SALAAM
         
Mwisho wa kutuma maombi kwa nafasi zote ni tarehe 27/02/2014


VACANCY ANNOUNCEMENT
The Principal Commissioner of Immigration Services announces vacant Posts in the Immigration Department.  Any Tanzanian Citizen with minimum qualifications mentioned hereunder is encouraged to apply:
A.      ASSISTANT INSPECTOR OF IMMIGRATION SERVICES (70 Posts)
  • Qualifications:
    • Tanzania Citizens aged not above 35 years
    • Holder of Bachelor Degree or Advanced Diploma from any University or Institution recognized by the Tanzania Government in the following disciplines:

Law, Economics, Business, Administration, Journalism, Education, Transportation, Human Resource, Computer Science, Information and Communication Technology, Statistics, Printing, Civil Engineering and Mechanical Engineering
  • Duties and Responsibilities:
  • To supervise patrols along the border areas, sea ports, bus stands, highways, railway stations, business centres and other entry points
  • To prepare charge sheets and prosecute in court all immigration related cases
  • To issue and receive various application forms for immigration services
  • To execute preliminary scrutinization of different application forms
  • To authorize opening of customers application files
  • To receive and scrutinize Passports and other travel documents
  • To authorise collection of government revenues for various immigration services
  • To keep records of all persons entering or leaving the country
  • To collect, organize and keep statistics of immigration and citizenship services
  • To notify customers in writing on the status of their applications

B.      CORPORAL OF IMMIGRATION SERVICES (100 Posts)
  • Qualifications:
    • Tanzania Citizens not above 30 years of age
    • Holder of Advanced Certificate of Secondary Education

C.      CONSTABLE OF IMMIGRATION SERVICES (100 Posts)
  • Qualifications:
    • Tanzania Citizens not above 25 years of age
    • Holder of Certificate of Secondary Education

D.      ADDED ADVANTAGES:
  • Certificate or Diploma in Law
  • Computer knowledge and typing
  • Full Technician Certificate (FTC) in Electricity and Mechanical Engineering
  • Certificate or Diploma in Secretarial duties
  • Certificate or Diploma in Records Management
  • Certificate or Diploma in Statistics
  • Certificate or Diploma in Marine Transport and Operations
  • Certificate in Trade Test Grade II, Advanced Drivers Course Grade II and Driving License Class C
  • Certificate or Diploma in Printing
  • Certificate or Diploma in Civil Engineering
  • Certificate or Diploma in Statistics
  • Duties and Responsibilities:

  • To conduct patrols along the border areas, sea ports, bus stands, highways, railway stations, business centres and other entry points
  • To conduct inspections in the hotels, guest houses and other business premises
  • To issue Immigration forms and information on the requirements for the services sought 
  • To escort immigration accused aliens/citizens in court
  • To escort deported aliens outside the country
  • To open and keep customers’ files in good order
  • To apprehend suspected immigration offenders
  • To make maintenance and regular service of equipment
  •   To collect, organize and keep immigration related statistics
NOTE: Selected applicants for the posts must attend a one year Basic Immigration Course prior to employment
D.      APPLICATION LETTERS MUST BE ACCOMPANIED WITH:
  • Two recent passport size photographs
  • Photocopy of Academic Certificates/Trainings
  • Photocopy of Birth Certificate
  • Letter of Introduction from Village/Ward Executive Officer or Sheha
  • Secondary/Advanced Secondary School Leaving Certificate
  • Primary school leaving Certificate
E.       MODE OF SUBMISSION
          All applications must be hand written and have to be submitted through Post Office
  • All applications for the post of Assistant Inspector of Immigration Services should be channeled to:

The Permanent Secretary,
Ministry of Home Affairs,
P.O. Box 9223,
DAR ES SALAAM
  • All applications for the post of Corporal and Constable of Immigration Services should be channeled to:

The Principal Commissioner of Immigration Services,
P.O. Box 512,
DAR ES SALAAM
Deadline for submission of applications: February 27, 2014.

No comments:

Post a Comment